SMZ kutumia teknolojia kuwanasa wanaokata misitu Zanzibar
Unguja. Kutokana na kasi ya ukataji misitu inayoendelea, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeandaa mpango wa kuanza kufuatilia na kudhibiti wanaokata misitu hiyo kwa njia ya kidijitali. Hayo yamebainishwa leo Machi 23, 2026 wakati wa kuadhimisha siku ya upandaji miti duniani ambapo kitaifa kwa Zanzibar imefanyika katika Shehia ya Muyuni, Wilaya ya Kusini, Mkoa…