Matatani tuhuma kuisababishia TTCL hasara ya Sh1.5 bilioni

Dar es Salaam. Mfanyabiashara na mkazi wa Moshi, mkoani Kilimanjaro, Grey Chilaza na mwenzake, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kulisababishia hasara ya Sh1.5 bilioni Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL ). Mbali na Chilaza, mshtakiwa mwingine ni Alex Ngonyani ambaye ni mkazi wa Mbinga mkoani Ruvuma. Washtakiwa hao…

Read More

Kamishna: Nidhamu, uadilifu ni msingi wa polisi

Morogoro. Jumla ya askari 785 wa Jeshi la Polisi wamehitimu mafunzo ya uongozi mdogo katika Chuo cha Maofisa wa Polisi Kidatu, huku wahitimu hao wakitakiwa kuzingatia haki za binadamu, nidhamu na uadilifu wanapotekeleza majukumu yao ya kazi. Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyowahusisha askari wa vyeo vya Sajini Meja (SM), Sajini Staff (SSGT) na…

Read More

JKT Queens, JKU kazi inaanza

BAADA ya jana kufunguliwa kwa michuano ya CECAFA ya wanawake kwa kuchezwa mechi mbili za makundi, CBE dhidi ya Rayon Sports na wenyeji Police Bullets dhidi ya Kampala Queens, leo saa 7:00 mchana JKT Queens itaikaribisha JKU Queens Zanzibar kwenye Uwanja wa Nyayo, Kenya.

Read More

Nsajigwa aanza hesabu za Yanga

BAADA ya kuanza na pointi moja dhidi ya Azam FC, Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa amesema hesabu zinahamia kwa Yanga kabla ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la CRDB dhidi ya TMA inayocheza  Championship. Nsajigwa aliyejiunga na maafande hao hivi karibuni kurithi mikoba ya Zedekiah Otieno, juzi aliiongoza timu hiyo ilitoshana nguvu dhidi…

Read More

Bado Watatu – 10 | Mwanaspoti

NIKAGEUKA na kumtazama mtu huyo aliyekuwa nyuma yangu na kumuuliza. “Ndiye yeye….amepatwa na nini sijui…?” “Inaonekana amejinyonga au amenyongwa.” “Ndiyo maana tangu jana sijamuona. Kumbe…!” Nikageuza uso tena na kuitazama ile maiti iliyokuwa inaning’inia. “Kama si wewe nisingetambua kama yeye ndiye Frank. Huyu jamaa anaishi na nani humu ndani?” “Anaishi peke yake. Aliwahi kuniambia kuwa…

Read More

SERIKALI KUSAIDIA ZAIDI SEKTA BINAFSI KUCHANGIA MAENDELEO YA KIUCHUMI InboxSearch for all messages with label Inbox

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(kulia) akiagana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Serengeti Breweries (SBL), Bw. Paul Makanza, baada ya kikao chake na ujumbe kutoka kampuni hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili umuhimu wa kudumisha mazingira thabiti na yanayotabirika…

Read More

Kuchelewa matibabu kunavyochangia bodaboda kukatwa viungo

Dodoma. Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI), wametaja sababu za wagonjwa wengi hasa madereva wa bodaboda au abiria wao kukatwa sehemu ya viungo vyao, ni kuchelewa kufika kwenye huduma. Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Machi 2, 2026 na Mkurugenzi wa MOI, Dk Mpoki Ulisubisya wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utendaji…

Read More