Mbunge wa Malava afariki akipatiwa matibabu Aga Khan
Nairobi. Mbunge wa Malava katika Kaunti ya Kakamega, Kenya, Moses Injendi amefariki dunia wakati akipatiwa na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan, Nairobi. Hayo yamethibitishwa na Spika wa Bunge Moses Wetang’ula jana Jumatatu Februari 17, 2025 bungeni “Waheshimiwa wabunge kwa huzuni ninawaarifu kuhusu kifo cha mwenzetu mheshimiwa Moses Malulu Injendi ambaye alituacha leo jioni (jana)…