Wawili wafariki dunia Kilimanjaro katika matukio mawili tofauti

Moshi. Mkazi wa Kijiji cha Kimbogho Kata ya Mamba Kusini Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Claudia Temba (68) amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kuteketea kwa moto ambao chanzo chake hakijafahamika. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo leo Jumanne Septemba 23, 2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema tukio hilo limetokea leo…

Read More

Simulizi ya mjane aliyetupiwa vitu nje Mikocheni

Dar es Salaam. “Kama shida ilikuwa hela, angesema marehemu mume wangu hakumlipa mimi ningejua namlipaje, lakini si kudai nyumba ni yake.” Ni kauli ya Alice Haule, mjane aliyefukuzwa kwenye nyumba anayodai ni yake iliyoko Mikocheni, Dar es Salaam, huku vitu vikitolewa nje. Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu akiwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala,…

Read More

Minja kukabili uhaba wa dawa akikinadi Chaumma Jimbo la Hai

Hai. Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Devota Minja ameahidi chama chake kitatua changamoto ya upatikanaji wa dawa katika hospitali na vituo vya afya nchini, ikiwamo katika Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro, kama kitapatiwa ridhaa ya kuongoza nchi. Akizungumza leo Jumanne Septemba 23, 2025  na wakazi wa Bomang’ombe katika mkutano…

Read More

Madaktari bingwa waweka kambi Maswa

Maswa. Madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando jijini Mwanza, wameweka kambi ya siku saba katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu kwa ajili ya kutoa huduma za matibabu ya kibingwa kwa wananchi wa maeneo hayo. Wananchi waliofika kupata huduma wamesema uwepo wa madaktari hao utawapunguzia gharama za kusafiri kwenda hospitali…

Read More

Zitto aahidi kuanza na barabara, Kata ya Businde

Kigoma. Mgombea ubunge wa Kigoma Mjini, kupitia chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema akishinda ubunge na wananchi wakampa madiwani wa chama hicho wataifungua Kata ya Businde kwa kuboresha miundombinu ya barabara. Akizungumza leo Jumanne, Septemba 23,2025 katika mkutano wa kampeni uliyofanyika Kata ya Businde, Zitto amesema kutokana na ubovu wa barabara ya kata hiyo wananchi…

Read More

Othman aahidi kukomesha mikopo kausha damu kwa walimu Zanzibar

Unguja. Mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, Othman Masoud Othman, amesema kuwa endapo atachaguliwa kuongoza dola ataanzisha mfuko maalumu wa maisha ya mwalimu, ili kuwaondolea  utegemezi wa mikopo yenye masharti magumu na isiyokuwa na tija kwa maisha yao. Othman ambaye ni Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo, amesema hayo leo Jumanne Septemba 23,2025 katika mkutano wake wa hadhara…

Read More

Kero ya maji kwa siku saba yamuibua RC Mtanda

Mwanza. Kwa zaidi ya wiki moja sasa wakazi wa baadhi ya maeneo ya Jiji la Mwanza wamekosa huduma ya maji baada ya pampu na vifaa vya kusambazia maji katika chanzo cha Butimba kuungua kutokana na hitilafu ya umeme. Changamoto hiyo imeathiri upatikanaji wa maji katika maeneo mbalimbali ikiwamo Mkuyuni, Buhongwa na Mkolani. Wakazi wa maeneo…

Read More

DC Nyamwese aanika fursa za uwekezaji Handeni

Na Augusta Njoji, Handeni TC MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, ametoa rai kwa sekta binafsi kuchangamkia fursa za biashara na uwekezaji katika sekta mbalimbali, ikiwamo viwanda vya kuchakata machungwa, ili kuchochea maendeleo ya wilaya hiyo. Akifungua kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya kilichofanyika mjini Handeni Septemba 23, 2025, Nyamwese ambaye pia…

Read More