Serikali yaingilia kati mgomo wa madereva daladala Himo
Moshi. Madereva daladala eneo la Njia Panda, Himo wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro, waligoma kwa zaidi ya saa tano wakidai madereva bajaji kuwanyang’anya abiria katika vituo vyao vya kupakia na kushusha abiria barabara ya Marangu–Mwika. Mgomo huo ulitokea Februari 25, 2026 na kusababisha usumbufu kwa wasafiri, huku daladala zikisitisha huduma zikishinikiza bajaji kuondoka katika eneo lao….