Skimu ya umwagiliaji kunufaisha wakulima 24,500 Mwanga
Mwanga. Wananchi wa Kata ya Kigonigoni, Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, wameiomba Serikali kuharakisha utekelezaji wa mradi wa skimu ya umwagiliaji unaoendelea katika eneo hilo, wakisema kukamilika kwake kutawasaidia kujikwamua kiuchumi na kupunguza umaskini. Mradi huo unatarajiwa kugharimu zaidi ya Sh16 bilioni na utanufaisha wakulima zaidi ya 24,500 katika kata hiyo, kwa kuongeza tija katika…