Mamia wajitokeza maziko ya Jenista, Dk Nchimbi akiongoza

Ruvuma. Mamia ya watu wamejitokeza katika kijiji cha Luanda kilichopo Halmashauri ya Mbinga mkoani Ruvuma, kwa ajili ya kuhitimisha safari ya mwisho ya aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama. Jenista ambaye amekuwa mbunge wa Peramiho kuanzia mwaka 2005, alifariki dunia Alhamisi, Desemba 11, 2025 jijini Dodoma, kwa matatizo ya ugonjwa wa moyo. Katika maziko…

Read More

WIZARA YA FEDHA KUSHIRIKIANA NA CHUO KIKUU MZUMBE KUIMARISHA USIMAMIZI WA MALI ZA SERIKALI.

Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma. Wizara ya Fedha, imeahidi kuendelea kushirikiana na Chuo Kikuu Mzumbe (MU) katika nyanja mbalimbali ikiwemo kujengeana uwezo katika masuala ya ununuzi, ugavi na usimamizi wa mali za Serikali ili kuandaa wahitimu waliobobea katika sekta hizo. Hayo yalibainishwa na Kaimu Naibu Katibu Mkuu Huduma za Hazina, Wizara ya Fedha, Bw. Lusius…

Read More

Kilimo ikolojia chatajwa kuongeza usalama wa chakula kwa walaji

Arusha. Matumizi makubwa ya kemikali, mbolea nyingi na dawa za kuulia wadudu yanayofanywa na wakulima nchini, yameelezwa ni chanzo cha uharibifu wa ardhi hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa usalama mdogo wa chakula. Matumizi hayo pia yameelezwa kuwa hayampi mkulima uhakika kupata mazao mengi licha ya kutumia dawa nyingi wakati wa kilimo, hivyo kushauriwa kulima…

Read More

Mashabiki Simba, Yanga kuonyeshana umwamba

Mashabiki wa Simba na Yanga watacheza mechi ya kirafiki, Jumapili, Desemba 21, 2025 kwa lengo la kuhamasisha upendo na umoja baina yao. Mechi hiyo itachezwa katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 10:00 jioni na hakutakuwa na kiingilio kwa mashabiki. Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amewaomba mashabiki wajitokeze kwa…

Read More