Mwalimu: Tutaibadili Uyole kuwa kitovu cha biashara Afrika
Mbeya. Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Salum Mwalimu, ameahidi kuwa endapo atachaguliwa katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, serikali yake itaanzisha mpango kabambe wa kuliboresha eneo la Uyole, mkoani Mbeya. Amesema ataboresha eneo hilo kwa kujenga kituo cha kimataifa kitakachokuwa mfano wa ukaribisho wa Tanzania kwa wageni kutoka…