Mawazo kinzani mkakati wa KKK ukianza kutekelezwa
Dar es Salaam. Kutengenezwa kwa Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa watoto wa elimu ya awali na wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili umeibua mjadala miongoni mwa wataalamu wa elimu, wakiwamo wale wanaoonesha wasiwasi kuwa unaweza kuwa mkakati mwingine mzuri kwenye makaratasi bila kutatua changamoto halisi…