Mashahidi 13 kutoa ushahidi, kesi ya kusafirisha kilo 51 za heroini
Dar es Salaam. Mashahidi 13 na vielelezo 16 vinatarajiwa kutolewa mahakamani katika kesi ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroini zenye uzito wa kilo 51.47 inayomkabili mkazi wa Kawe, Ernest Semayoga (48) na wenzake watatu. Mbali na Semayoga maarufu Mukri na washtakiwa wengine ni mfanyabiashara Salum Jongo (45) mkazi wa Mbezi Beach, Amin Kesibo…