Mgaza atupia mbili Dodoma Jiji ikiibonda Coastal Union

MSHAMBULIAJI wa Dodoma Jiji, Yassin Mgaza, ameendeleza moto wa kucheka na nyavu katika mashindano ya Tanzanite Pre-Season International baada ya kufunga mabao mawili dhidi ya Coastal Union. Mgaza ambaye amefikisha mabao matatu na kuwa kinara wa ufungaji kwenye michuano hiyo, alianza kuziona nyavu za Coastal Union mapema tu dakika ya pili akiitumia vizuri pasi ya…

Read More

Mgombea mwenza Chaumma akerwa utitiri wa kodi, ushuru kwenye mazao, aahidi neema

Morogoro. Mgombea mwenza urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Devotha Minja amewahakikishia Watanzania endapo chama hicho kitaingia madarakani kero ya tozo za mazao ya kilimo na utitiri wa kodi kwa wafanyabiashara zitaondolewa. Amesema Serikali ilipaswa kuwawezesha wakulima kwa zana bora za kilimo  na sio kusubiri wakulima kuteseka kulima, kuvuna na baadae kudaiwa ushuru….

Read More

CCM Kinondoni kuanza na makundi kisha kampeni

Dar es Salaam. Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, kimesogeza mbele ratiba ya kuanza kampeni zake kikisema kinatoa nafasi ya kuvunja makundi yaliyoibuka kipindi cha kura za maoni. Kampeni rasmi katika majimbo ya Kawe na Kinondoni zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi Septemba 13 na 14, 2025, kama sehemu ya maandalizi kuelekea Uchaguzi…

Read More

Mwalimu aahidi utajiri kwa vijana akiingia Ikulu

Tanga. Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Salum Mwalimu ameahidi iwapo atachaguliwa kuwa rais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, atahakikisha vijana wa Kitanzania wanakuwa matajiri kupitia njia halali na endelevu. Ameyasema hayo leo Jumanne Septemba 2, 2025 wakati akihutubia wananchi wa kata za Maramba na Mapatano wilayani…

Read More

Mati Technology Yapanua Wigo wa Kilimo kwa Teknolojia ya Drone

Na Mwandishi Wetu. KAMPUNI ya Mati Super Brands Ltd kupitia tawi lake la Mati Technology imezindua teknolojia mpya ya ndege nyuki (drone) zinazotengenezwa nchini, zenye uwezo wa kuboresha sekta ya kilimo na huduma nyingine za kijamii. Mkurugenzi Mtendaji wa Mati Group of Companies, David Mulokozi, amesema kampuni hiyo imeamua kuwekeza katika uzalishaji wa drone zinazotumika…

Read More

Dk Slaa: Kampeni za uchaguzi hazijagusa masuala muhimu

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema kampeni za uchaguzi wa mwaka huu, zimekosa chama kinachozungumza masuala muhimu kwa raia. Dk Slaa anasema hayo, wakati chama chake kikiwa si miongoni mwa vinavyoshiriki uchaguzi kutokana na ajenda yake ya kudai mabadiliko mifumo ya uchaguzi maarufu…

Read More