
NDIYO MILIONI 20 ZA HESLB ZITAKAVYOSAIDIA KUBORESHA MASOMO YA SAYANSI NCHINI
::::::: Na: Dkt. Reubeni Lumbagala, Tanga Juhudi zinazofanywa na serikali katika kuchochea maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla haziwezi kuzaa matunda kama hakutafanyika uwekezaji wa kutosha katika sekta ya elimu. Hii inatokana na ukweli kuwa maarifa, ujuzi na stadi mbalimbali ni nyenzo muhimu zinazoharakisha kufikiwa kwa malengo na mipango ya maendeleo. Kwa kuzingatia ukweli…