Waliohukumiwa kunyongwa kwa mauaji ya bodaboda waachiwa huru
Arusha. Mahakama ya Rufani imebatilisha adhabu ya kunyongwa hadi kufa iliyokuwa imetolewa dhidi ya Hamis Ernest na Renatus Simon, waliokuwa wamepatikana na hatia ya kumuua dereva wa bodaboda, Gervas Genus. Kuachiwa kwao kumetokana na Mahakama ya Rufani kubaini kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha shitaka hilo bila kuacha shaka. Uamuzi huo umetolewa Februari 27, 2026…