Ibenge kuifikisha Azam nchi ya ahadi?
TANGU msimu wa 2013-14 ambao Azam FC ilibeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara ikiwa ni mara ya kwanza kwao, wamepita makocha mbalimbali kuifukuzia rekodi hiyo, wameshindwa. Mzigo huo sasa umeangukia kwa Florent Ibenge, kocha mwenye rekodi kubwa katika soka la Afrika kutokana na kushinda mataji yanayosimamiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF). Ibenge…