Profesa Mahalu afariki dunia, aacha historia
Dar es Salaam. Profesa wa sheria na mwanadiplomasia nguli, Profesa Costa Mahalu (77) amefariki dunia. Taarifa kutoka kwa familia yake imethibitisha Profesa Mahalu amefariki dunia leo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) alikokuwa akipatiwa matibabu. Hadi anafariki dunia, Profesa Mahalu alikuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu St Augustine akiendelea kutoa elimu ya sheria. …