Nyuki walioweka makazi Msamvu watimka na kung’ata watu

Morogoro. Baadhi ya watumiaji wa vyombo vya moto, baiskeli na watembea kwa miguu wameng’atwa na nyuki waliokuwa wamevamia eneo la Msamvu Mataa, Manispaa ya Morogoro, huku wengine wakipata majeraha baada ya kudondoka na vyombo vyao vya usafiri wakijaribu kuwakimbia nyuki hao. Tukio hilo limetokea leo Jumatano Septemba 10 kwenye nguzo za taa za barabarani zilizopo…

Read More

Gor Mahia katikati ya mtego wa Simba

WAKATI tamasha la kilele la Simba Day likihitimishwa leo, kikosi cha Gor Mahia ya Kenya kiko katika mtego wakati kikiwa nyuma kwa bao 1-0 dhidi ya ‘Wekundu hao wa Msimbazi’. Iko hivi, mara ya mwisho kwa Simba kupoteza mechi ya Simba Day dhidi ya timu kutoka Kenya ilikuwa mwaka 2012, jambo linalosubiriwa kuona kama Gor…

Read More

Simba Day yamkosha BM3, ampigia chapuo Mghana mwenzie

NYOTA wa zamani wa Simba raia wa Ghana, Bernard Morrison ‘BM3’, amesifu tamasha la kikosi hicho linalofanyika leo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram, Morrison aliandika ‘Hili ndilo tukio langu bora kwa leo Tanzania, lenye mandhari ya ajabu, Simba Day.” Hata hivyo, licha…

Read More

Dk Nchimbi aeleza sababu CCM kuomba ichaguliwe tena

Katavi. Mgombea mwenza wa urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk Emmanuel Nchimbi amesema mafanikio makubwa yaliyopatikana miaka mitano iliyopita, yanakifanya chama hicho kutoka kifua mbele kuomba tena ridhaa ya Watanzania kuwaongoza. Amesema maeneo mbalimbali nchini kuna miradi mingi imekamilika au inaendelea kutekelezwa mathalani ya afya, elimu, barabara, kilimo, ufugaji, uvuvi na maji inayochochea uchumi…

Read More

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUTOA AJIRA MALIASILI NA UTALII

……………. Na Sixmund Begashe, Mwanza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutoa fursa ya ajira kwa vijana waliohitimu vyuo vilivyopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu (Uhifadhi) wa Wizara hiyo, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba, katika mahafali ya 61 ya Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi…

Read More

Serikali ya Chaumma kupambana na madalali wa tumbaku

Kaliua. Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) kimesema endapo kitaingia madarakani, kitahakikisha wakulima wa tumbaku wanapata manufaa halisi ya kilimo hicho kwa kuondoa changamoto zinazowakwamisha, ikiwamo udhibiti wa madalali wanaowanyonya. Chama hicho pia kimeahidi kuweka mifumo bora ya ununuzi wa tumbaku na kuhakikisha bei ya mazao inaakisi gharama halisi za uzalishaji ili kuongeza tija kwa…

Read More

Arusha warudisha hadhi ya marathoni

MKOA wa Arusha umeanza mkakati wa kurudisha hadhi ya riadha baada ya kutangaza kuwa mbio za Tanfoam zifanyika zikitumia umbali wa kilomita 42. Arusha ndiyo waanzilishi wa mbio ndefu za kilomita 42 na awali zilijulikana kuwa Mount Meru Marathon ambazo zilikuwa za kwanza kuwa na hadhi ya kimataifa kwa kuleta wanariadha nyota sehemu mbalimbali. Mount…

Read More

ADC yaahidi mapinduzi ya kilimo, mikopo, miundombinu na kodi

Simiyu. Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaoa kupitia Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Wilson Mulumbe, ameahidi kujenga kiwanda cha vifaa tiba mkoani Simiyu kwa lengo la kuongeza thamani ya zao la pamba, endapo kitashinda katika uchaguzi mkuu ujao. Akizungumza leo, Jumatano, Septemba 10, 2025, mjini Bariadi, Mulumbe amesema lengo la kiwanda…

Read More