Neema arejea nchini na ubingwa wa Perm Marathon
Mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania, Neema Msuadi amerejea nchini akitokea Russia alikokwenda kushiriki mbio za Perm Marathon. Mbio hizo zilifanyika Oktoba, mwaka huu, jijini Perm ambako Neema alimaliza wa kwanza kwa muda wa saa 2:38:15 na kuwa Mtanzania wa pili kuongoza mwaka huu baada ya Gabriel Geay kufanya hivyo mwezi Februari akishinda Daegu Marathon za…