Mwanafunzi aliyeuawa, mwili kuchomwa Mbeya azikwa
Mbeya. Mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Mbeya, Shyrose Mabula, aliyeuawa kikatili kisha kuchomwa moto, umezikwa, huku waombolezaji wakipaza sauti kukemea tukio hilo, wakitaka wahusika wapatikane na kuchukuliwa hatua za kisheria. Maziko yamefanyika leo, Septemba 20, 2025, katika Makaburi ya Iwambi, mkoani Mbeya. Shyrose (21) alikutwa ameuawa, kisha mwili kuchomwa moto…