Miili sita ya wahamiaji yaopolewa baharini

Roma, Italia. Walinzi wa pwani ya Italia wamesema wameopoa miili sita baada ya boti ya wahamiaji kuzama wiki hii kwenye pwani ya Kusini ya Bahari ya Mediterania, huku zaidi ya watu 60 wakiripotiwa kutoweka wengi wao wakiwa ni watoto. Shirika la Habari la AFP limesema watu 12 wameokolewa baada ya mashua hiyo kuzama karibu maili…

Read More

THPS YATOA ELIMU KWA WAHARIRI NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU HUDUMA ZA AFYA ZINAZOTOLEWA KUPITIA MRADI WA CDC/PEPFAR AFYA HATUA

      Mkurugenzi wa Huduma za Jamii wa Shirika la THPS, Dkt. Appolinary Bukuku akizungumza wakati akifungua kikao kazi cha siku mbili kati ya THPS na Wahariri na Waandishi wa Habari kilichofanyika Jijini Tanga. Mkurugenzi wa Huduma za Jamii wa Shirika la THPS, Dkt. Appolinary Bukuku akizungumza wakati akifungua kikao kazi cha siku mbili…

Read More

Kampuni sita za Kitanzania zaonyesha nia kuendesha SGR

Dar es Salaam. Kampuni sita za Kitanzania ni miongoni mwa kampuni kadhaa ambazo zimeonyesha nia ya kushirikiana na serikali katika kuendesha Reli ya Standard Gauge (SGR). Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa kufuatia kutangazwa kwa Kanuni za Matumizi ya Miundombinu ya Reli kwa Watoa Huduma Binafsi za mwaka…

Read More

Dk Mpango aeleza ya kukumbukwa kwa RAS Kilimanjaro

Moshi.  Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango amesema Serikali imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Tixon Nzunda aliyefariki dunia Juni 18, 2024 kwa ajali ya gari, huku akieleza alikuwa mtu makini katika utendaji kazi. Nzunda (56) na dereva wake Alphonce Edson (54) walifariki dunia jana Juni 18, 2024…

Read More

Mamia ya mahujjaji wafa Makka kwa joto kali – DW – 19.06.2024

Saudi Arabia haijazungumzia idadi ya vifo hivyo vilivyotokea katikati mwa joto kali wakati wa hijja, wala kutoa sababu zozote kwa waliofariki, lakini mamia ya watu walikuwa wamejipanga kwenye Jengo la Dharura katika kitongoji cha Al-Muaisem mjini Makka, wakijaribu kupata taarifa kuhusu wanafamilia wao waliopotea. Orodha moja inayosambaa mtandaoni iinaonyesha takriban watu 920 walikufa wakati wa…

Read More

Wafungwa, mahabusu walioko magerezani kusajiliwa Nida

Dodoma. Serikali itaanza kusajili vitambulisho vya Taifa kwa wafungwa na mahabusu walioko magerezani katika mwaka 2025/26. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Daniel Sillo amesema hayo leo Juni 19, 2024 wakati wakijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Asia Halamga. Asia amehoji Serikali ina mpango gani kuwapa vitambulisho vya Taifa wafungwa pamoja na mahabusu….

Read More