WANANCHI KITOMONDO WAIOMBA SERIKALI KUINGILIA MGOGORO WA ARDHI WA MIAKA 20
Na Emmanuel Mbatilo, Kibaha Wananchi wa Kijiji cha Kitomondo, wilayani Kibaha mkoani Pwani, wameiomba Serikali kuingilia kati mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 20 kati yao na mfugaji anayedaiwa kumiliki eneo la takribani hekari 7,000. Eneo hilo linaelezwa kuenea hadi wilaya jirani ya Kisarawe na kusababisha wananchi kukosa maeneo ya kutosha kwa ajili…