Dk Nchimbi alivyomaliza mvutano wa Matiko, Kembaki
Rorya/Tarime. Mvutano wa kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Jimbo la Tarime Mjini limechukua sura mpya baada ya mgombea mwenza wa urais wa chama hicho, Dk Emmanuel Nchimbi kuumaliza kwa kumteua, Michael Kembaki kuwa kampeni meneja wa Esther Matiko. Kembaki alikuwa mbunge wa jimbo hilo (2020-2025), katika kura za maoni mwaka huu aliongoza, lakini…