Aliyeshtakiwa kwa kula, kulala Hoteli ya Serena bila kulipa afutiwa kesi

Dar es Salaam. Mahakama ya Mwanzo Kariakoo imemfutia kesi na kumwachia huru mfanyabiashara aliyeshtakiwa kwa kujipatia huduma ya chakula na malazi katika Hoteli ya Serena kwa njia ya udanganyifu. Mshtakiwa Denis Mfumbulwa (44) alidaiwa kujipatia huduma hizo zenye thamani ya Sh21.4 milioni bila kulipa, akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria. Mfumbulwa amefutiwa kesi Mahakama ikieleza…

Read More

Biashara ya mkaa pasua kichwa, yafikia Sh69.9 bilioni

Wakati dunia ikiendelea kupigia chapuo matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa ajili ya kulinda mazingira, hali bado ni tete kwa upande wa Tanzania, ambayo uuzaji wa mkaa umeongezeka kwa karibia mara 20 zaidi ndani ya mwaka mmoja. Tanzania imekuwa kinara wa kampeni ya matumizi ya nishati safi ya kupikia barani Afrika. Mara kadhaa Rais…

Read More

Bajeti ya uchaguzi, kulinda haki za raia

Dodoma. Nyongeza ya fedha kwenye bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani, imelenga kuwezesha utekelezaji wa mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai. Pia bajeti hiyo imelenga kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kutimiza majukumu yake, ikiwemo la uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu mwakani. Maombi ya…

Read More

Hali ya utulivu imeanza kurejea Kharkiv – DW – 16.05.2024

Zelensky amesema aliyevamia mkoa huo wa Kharkiv ataangamizwa kwa namna yoyote na kwa kutumia rasilimali zilizopo, huku akisifu ufanisi wa vikosi vyake na kusisitiza kuwa wanaendeleza pia mapambano katika mji wa Kupyansk, katika mkoa wa Donetsk na pia katika mji wa Vovchansk karibu na mpaka wa Urusi. Rais Zelensky ambaye amelazimika kuahirisha safari zake zote…

Read More

Apandishwa kizimbani akidaiwa kumbaka mtoto wa miaka 17

Geita. Mkazi wa Mgusu Mjini Geita Magongo Kulwa (30) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Geita akidaiwa kumbaka mtoto wa miaka 17.  Mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo, Nyakato Bigirwa, Mwendesha mashtaka Luciana Shaban amesema mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 4, 2024 huko Mgusu. Hata hivyo, mshtakiwa huyo alikana kutenda kosa hilo na…

Read More

Mbunge aliyetaka pasipoti kuingia Zanzibaar azua jipya

Dodoma. Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo), Mohamed Said Issa aliyetaka wananchi wa Tanzania Bara (Watanganyika) waingie Zanzibar kwa pasipoti, amezua lingine la ubaguzi akikataa taarifa tatu za kumtambua yeye ni Mtanzania. Hayo yametokea bungeni leo Mei 15, 2024 wakati wa mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani kwa mwaka wa…

Read More