Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Septemba 25, 2025
Nafasi za kazi kila siku Tanzania, Serikalini, Makampuni na Taasisi mbalimbali tembelea website yetu ya Global Publishers muda wote bonyeza hapa Publishers muda wote bonyeza hapa
Nafasi za kazi kila siku Tanzania, Serikalini, Makampuni na Taasisi mbalimbali tembelea website yetu ya Global Publishers muda wote bonyeza hapa Publishers muda wote bonyeza hapa
Mikoani. Ni kicheko na maumivu kwa wagombea wa nafasi ya ubunge na udiwani baada ya baadhi kuteuliwa na wengine kukosa sifa ya kuteuliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kuanza safari ya kusaka kura kuwaongoza wananchi ngazi ya kata na jimbo. Wagombea wa ubunge Jimbo la Moshi Vijijini kutoka chama Makini na Jimbo…
Mtwara. Katika juhudi za kuendelea kuwezesha vijana jukwaa la vijana nchini limezinduliwa mkoani Mtwara limefunguliwa mahususi kutoa elimu ya fedha na mafunzo ya ujasiriamali yatakayowasaidia kujishughulisha kiuchumi na kujiingizia kipato. Ufunguzi wa jukwaa hilo linalowaunganisha vijana nchi nzima ni mwendelezo wa jitihada za Serikali kwa kushirikiana na CRDB Bank Foundation. Katika uzinduzi huu ulioongozwa na…
Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia CCM, amewasili Unguja akitokea Pemba kufuatia msiba mzito wa kaka yake, Mhe. Kapteni Abbas Ali Mwinyi, aliyefariki dunia leo tarehe 25 Septemba 2025 katika Hospitali ya Lumumba, Unguja. Marehemu Kapteni…
WAKATI mashabiki wa Simba wanasubiri kwa hamu kumuona Mohammed Bajaber akiichezea timu hiyo kwa mara ya kwanza katika mechi za mashindano, kocha wa zamani aliyewahi kumnoa wakati akiwa Polisi Kenya, amempa ‘code’ kocha Fadlu Davids aweze kumfaidi vyema kikosini. Bajaber ni kati ya…
Moshi. Asilimia mbili pekee ya taasisi za umma zinatumia nishati safi ya kupikia mkoani Kilimanjaro, taarifa ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imeonyesha. Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034), Sura ya Nne, sehemu ya viashiria vya matokeo uliweka: “Katazo la matumizi ya kuni na mkaa wa asili katika taasisi 31,395…
WADAU wa maendeleo, wasomi na wataalamu kutoka sekta binafsi na uma wamesema Tanzania imepiga hatua kupitia Dira 2025 licha ya changamoto za kiuchumi za kimataifa huku wakitaja kuwa kilimo bado ni sekta dhaifu kutokana na utegemezi wa mvua na ukosefu wa viwanda vya zana za kilimo na kushauri kuongezwa uwekezaji katika umwagiliaji, miundombinu ya uchumi…
Na Mwandishi Wetu USHIRIKIwa Tanzania katika maonesho makubwa ya utalii duniani ITB Berlin nchini Ujerumani, umeelezwa kuwa wa mafanikio makubwa, huku ukitoa fursa pana ya kuitangaza nchi kama kitovu cha utalii barani Afrika na kufungua milango mipya ya biashara na uwekezaji katika sekta hiyo muhimu ya uchumi. Mafanikio hayo yanatokana maonesho ambayo yanafanyika kila mwaka…
WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umetangaza kuanza oparesheni ya kuwaondoa wadaiwa sugu katika nyumba za Serikali kuanzia Oktoba 1, mwaka huu endapo watashindwa kulipa kodi zao za pango hadi Septemba 30. Wito huo umetolewa leo Septemba 10, 2025 Jijini Dar es Salaam na Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daud Kondoro, alipokuwa akizungumza na waandishi wa…