
Kwa nini waishiwa wasiwe madoktari au wabukuzi
Kaya yetu si ya watata wala haihitaji utata, kuringa, na kuringishiana ujuha. Ni kaya ya mafyatu. Hii inatosha. Siku hizi, kila fyatu anataka aitwe ama doktari au profedheha hata kama hajui kusoma na kuandika ilimradi tu ujiko na kujimwambafy. Hawajui wanavyotusononesha sie tusiobahatika kuwa madoktari wala maprofedheha ingawa ukiwauliza wamefanya nini cha mno, wote ngoma…