
Simulizi wanayokumbana nayo wanawake wauza ndizi mtaani
Moshi. Wakati baadhi ya watu wakiitazama biashara ya ndizi mbivu mitaani kama ya kimasikini, ukweli ni kwamba biashara hiyo imekuwa mkombozi kwa wanawake wengi katika Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro. Biashara hiyo imewapa mafanikio kama vile kujenga nyumba, kusomesha watoto, kusaidia familia zao mahitaji muhimu ya kila siku huku wakijisikia furaha kuifanya kama ajira inayoendesha…