FYATU MFYATUZI: Nimeamua kujipanga kuuza au kubinafsisha ubongo wangu!
Sihitaji ubongo tena. Kwanza, umenifyatua nikafyatua wengine hadi wanatishia kunifyatua kwa kuninyotoa roho. Ubongo umesababishe kero na hatari hadi nikageuka machukizo, ukiachia kujiudhi mwenyewe. Ubongo umenibomoa badala ya kujijenga. Nilifyatua wengine ili wafyatuke na kuwafyatua wanaowafyatua nikaishia kujibomoa. Mbali na ubongo kuniletea madhara kwa vile unachemka, zipo sababu zilizoko nje ya uwezo wangu zinazoniaminisha kuwa…