Kocha CBE asepa na somo CECAFA

KOCHA wa CBE, Birhanu Gizaw amesema msimu huu haukuwa mzuri kwa upande wao wakikutana na ushindani mkubwa kwenye mashindano ya CECAFA ya kuwania kufuzu ushiriki wa Ligi ya Mabingwa Afrika kwa Wanawake. Mabingwa hao watetezi wa CECAFA waliishia katika hatua ya makundi baada ya kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Kundi B, wakianza kwa kupoteza…

Read More

UN inakaribisha tukio kubwa zaidi la haki za wanawake duniani – Masuala ya Ulimwengu

Wakati mwaka huu Siku ya Kimataifa ya Wanawakeinayoadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi, inaangazia haki, mifumo inayokusudiwa kuwalinda wanawake na wasichana inashindwa, huku mamilioni wakikabiliwa na ubaguzi, unyanyasaji na kutoadhibiwa huku upinzani dhidi ya usawa wa kijinsia ukiongezeka na ukiukwaji wa haki za msingi kuongezeka duniani kote, kulingana na ripoti mpya iliyotolewa kutoka UN Women….

Read More

Sekondari ya Temeke yapigwa tafu vifaa vya maabara

Dar es Salaam. Katika kutekeleza mkakati wa kuinua ubora wa elimu ya sayansi nchini Tanzania, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa msaada wa Sh10 milioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya maabara katika Shule ya Sekondari Temeke. Fedha hizo zimekabidhiwa shuleni hapo, kwa ajili ya kununua vifaa vya maabara…

Read More

Marekani kurudisha miradi ya USAID Tanzania

Arusha. Ubalozi wa Marekani nchini umethibitisha kuwa miradi ya maendeleo iliyokuwa ikitekelezwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) itarejeshwa, licha ya shirika hilo kufungwa mapema mwaka huu. Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili, Septemba 14, 2025, na Balozi wa muda wa Marekani nchini, Andrew Lentz, alipozungumza na waandishi wa habari jijini Arusha baada…

Read More

Puma yaboresha upatikanaji wa nishati Singida

Dar es Salaam. Kampuni ya Puma Energy imezindua kituo cha huduma mkoani Singida, ikisema hatua hiyo inalenga kuboresha upatikanaji wa nishati, kuunda fursa za kiuchumi na kutoa huduma za kisasa kwa wananchi. Kituo hicho kipya kimeelezwa kitachangia kukuza maendeleo ya kiuchumi ya mkoa huo na maeneo ya jirani. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho,…

Read More

Aliyeanza na mtaji wa elfu mbili, apewa Sh5 milioni, kiti mwendo

Sengerema. Baada ya dhiki, faraja. Ndivyo ilivyokuwa kwa mkazi wa Sengerema aliyepata ulemavu wa kudumu baada ya kudondokewa na kifusi mgodini, lakini akaanza kujiajiri kwa kushona viatu kwa mtaji wa Sh2,000. Mwananchi huyo alikuwa miongoni mwa walioudhuria mkutano wa hadhara wa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi uliofanyika…

Read More

Mgaza atupia mbili Dodoma Jiji ikiibonda Coastal Union

MSHAMBULIAJI wa Dodoma Jiji, Yassin Mgaza, ameendeleza moto wa kucheka na nyavu katika mashindano ya Tanzanite Pre-Season International baada ya kufunga mabao mawili dhidi ya Coastal Union. Mgaza ambaye amefikisha mabao matatu na kuwa kinara wa ufungaji kwenye michuano hiyo, alianza kuziona nyavu za Coastal Union mapema tu dakika ya pili akiitumia vizuri pasi ya…

Read More