Dk ‘Manguruwe’ afikisha siku 287 rumande, upelelezi bado

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Kampuni ya Vanilla International Ltd, Simon Mkondya (40), maarufu Dk Manguruwe, amefikishwa siku 287 akiwa rumande kutokana na upelelezi wa kesi yake ya uhujumu uchumi, kutokamilika. Mkondya na mwenzake, Rweyemamu John (59), ambaye ni Mkaguzi wa fedha wa kampuni hiyo, wanakabiliwa na mashtaka 28 yakiwemo ya kuendesha biashara ya upatu…

Read More

Jussa: Hatuafiki kura ya mapema, chama kitatoa mwongozo

Unguja. Siku moja baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kueleza kuendelea kutumika utaratibu wa kawaida wa kura ya mapema, Chama cha ACT-Wazalendo kimewataka wananchi kisiwani humo watulie na suala hilo litashughulikiwa na viongozi wa chama hicho. Hayo yameelezwa leo Jumanne, Agosti 19, 2025  na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Ismail Jussa wakati akifungua kikao…

Read More

Wazawa washirikiana na wageni kuleta neema ubanguaji korosho

Mtwara. Ili kufanikisha malengo ya kuongeza kiwango cha korosho kinachobanguliwa nchini Kampuni ya South Saharan Engineering Limited (SSEL) na Akros Limited kwa kushirikiana na wawekezaji wa kigeni wanatarajia kujenga kiwanda cha kuzalisha mashine za kubangua zao hilo. SSEL inatarajia kushirikiana na kampuni ya JohnCashew Mashine kutoka nchini Vietnam, kiwanda kinatarajiwa kujengwa mkoani Mtwara eneo ambalo…

Read More

Mafuriko yaua watu watatu, yaacha zaidi ya 100 bila makazi

Kampala. Watu watatu wamefariki dunia huku zaidi ya watu 100 wakipoteza makazi baada ya mafuriko makubwa kuyakumba maeneo ya Mbale na Sironko nchini Uganda. Taarifa iliyotolewa na tovuti ya habari ya Daily Monitor ya Uganda imeeleza kuwa mafuriko hayo yamesababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha tangu Jumapili, Agosti 17, 2025, na kusababisha uharibifu wa miundombinu…

Read More

Jaji Mkuu akemea watuhumiwa kunyimwa dhamana

Dodoma. Jaji Mkuu wa Tanzania, George Masaju amekemea tabia ya baadhi ya mahakimu kuwanyima dhamana watuhumiwa ambao kesi zao zinadhaminika akisema kitendo hicho ni kiashiria cha kutaka rushwa. Jaji Masaju amesema kesi yoyote ambayo inaangukia katika kifungu cha dhamana, ni muhimu watuhumiwa wakapewa siku hiyohiyo ili kukwepa msongamano magerezani na ataanza kulifuatilia jambo hilo mwenyewe….

Read More

Suti ya kijeshi ya Zelenskyy yazua mjadala

Dar es Salaam. Baada ya kusakamwa kutovaa suti kwenye mkutano wa Rais Donald Trump uliopita, Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy hatimaye katika mkutano wa jana wa kutafuta amani ya Ukraine na Russia, alionekana amevaa suti ya kijeshi hatua iliyoibua mada mpya. Katika mkutano uliopita mapema mwaka huu kati ya Trump na Zelenskyy na Makamu wa…

Read More