UCHAMBUZI WA MALOTO: CUF 2025 inamtoa chozi Seif kaburini, Profesa Lipumba akishika tama
Agosti 31, 2025, Viwanja vya Furahisha, Mwanza, ulifanyika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za mgombea urais wa Chama cha Wananchi (CUF), Gombo Samandito Gombo. Hali ya mkutano inatafakarisha. Inasikitisha. Mahudhurio ya watu yalikuwa kidogo. Hadhira ilitosha hema moja. Kila kitu kilidhihirisha jinsi chama hicho kilivyo na uhaba wa rasilimali. Mtu mgeni na asiyejua historia, angeadhani…