Mwalimu mkuu, mlinzi mbaroni tuhuma za kumfanyia ukatili mwanafunzi
Arusha. Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ngarenaro, Mussa Luambano (50) na mlinzi wa shule hiyo, Olais Mollel (33), wakituhumiwa kumfanyia ukatili mwanafunzi wa darasa la saba. Akitoa taarifa leo Septemba 3, 2025 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema watuhumiwa wanadaiwa kutumia mnyororo na kufuli, kumfunga mguu…