Tanzania Mnufaika wa Mpango wa TEF wa Ujasiriamali Afrika 2026
Tanzania imepata uwakilishi miongoni mwa wanufaika wa Mpango wa Ujasiriamali wa Taasisi ya Tony Elumelu (TEF) wa mwaka 2026, huku wajasiriamali 12 wakichaguliwa katika kundi la kwanza la washindi waliotangazwa barani Afrika. Hayo yalitangazwa Transcorp Hilton Abuja, ambapo wajasiriamali 1,951 walibainishwa kama sehemu ya wanufaika wapatao 3,200 watakaosaidiwa na TEF kwa mwaka huu. Uteuzi huo…