Ambokile atuliza presha Mbeya City
MSHAMBULIAJI wa Mbeya City, Eliud Ambokile amesema licha ya mwenendo usioridhisha wa kikosi hicho msimu huu katika Ligi Kuu Bara, lakini bado wana nafasi ya kubadilisha upepo mbaya unaowaandama, kutokana na ubora wa wachezaji waliopo kikosini. Akizungumza na Mwanaspoti, Ambokile, alisema bado wana wachezaji wazuri wanaoweza pia kubadilisha hali iliyopo, licha ya ushindani mkali uliopo…