Serikali kuboresha bandari za Kibirizi, Ujiji
Dodoma. Serikali imesema imeanza utekelezaji wa hatua za kurejesha bandari za Kibirizi na Ujiji mkoani Kigoma zilizokumbwa na athari za mabadiliko ya tabianchi kutokana na kuongezeka kwa kina cha maji katika Ziwa Tanganyika, hali iliyosababisha kudorora kwa shughuli za usafirishaji na biashara. Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumanne, Februari 3, 2026, na Naibu Waziri wa…