Dili jipya la Dube, Wasaudia, Morocco wakitia timu Yanga
WAKATI mkataba wa mshambuliaji wa Yanga, Prince Dube ukielekea ukingoni, mabosi wa klabu hiyo wameanza hesabu mapema za kuhakikisha staa huyo hachomoki Jangwani. Dube aliyetua Yanga mwanzoni mwa msimu wa 2024-2025 akitokea Azam, alisaini mkataba wa miaka miwili kukitumikia kikosi hicho unaomalizika Juni 2026. Mwanaspoti linafahamu kuwa, baada ya Dube kucheza michuano ya AFCON 2025…